• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAPITISHA RASIMU YA BAJETI ZAIDI YA BILIONI 93.5

Posted on: February 8th, 2025

BARAZA la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Geita Februari 7, 2025 katika Mkutano wake Maalum uliofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri-Nzera limepitisha rasimu ya Bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/2026 kiasi cha Shilingi Bilioni 93.5

Awali akiwasilisha mapendekezo ya mpango na bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/2026 kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji, Afisa Mipango wa Halmashauri Bi Sarah Yohana amesema Halmashauri ya Wilaya ya Geita inapendekeza kukusanya na kutumia jumla ya Tsh Bilioni 93.5 ambapo  kiasi cha Tsh Bilioni 16.5 ni fedha za ruzuku zitakazotumika kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo.

Aidha Bi Sarah ameongeza kwa kusema katika bajeti hiyo kiasi cha Tsh Bilioni 1.5 ni ruzuku zitakazotumika kwa matumizi ya kawaida, Tsh Bilioni 63.5 zitatumika kwa ajili ya kulipa mishahara ya watumishi huku kiasi cha Tsh Bilioni 11.9 ni mapato ya ndani.

Afisa Mipango wa Halmashauri Bi Sarah Yohana akiwasilisha Rasimu ya Bajeti  kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji katika mkutano maalum wa Baraza la madiwani wa kujadili mapendekezo ya mpango na Bajeti kwa Mwaka 2025/2026

Akizungumza katika Baraza hilo Mwenyekiti wa  Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe Charles Kazungu amelipongeza Baraza la Madiwani kwa kupitisha bajeti hiyo ya kiasi cha Shilingi Bilioni 93.5

“Niwapongeze watumishi wetu chini ya Mkurugenzi makini bingwa kabisa Karia Rajabu Magaro kwa uandaaji mzuri wa bajeti yetu ya 2025/26 mmeandaa vizuri” amesema Mhe Kazungu.

Mhe Kazungu ametoa rai kwa watumishi na waheshimiwa madiwani kuendelea kuwa na ushirikiano ili kufikia lengo la bajeti hiyo. “Tuendelee kukaza buti  ili tufikie malengo ya makusanyo na kuvuka  asilimia za makusanyo, tuendelee kushikamana katika bajeti hii tunayoendelea nayo ili tuvuke lengo moto tuliokuwa nao usizimike” Ameongeza Mhe Kazungu.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe. Charles Kazungu akizungumza katika mkutano maalum wa Baraza la Madiwani wa kujadili mapendekezo ya Mpango na Bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/2026

Vilevile Mhe Kazungu amesema lengo  la Bajeti hiyo  ni kwenda kuwatumikia wananchi kwa kuwa  jiografia ya Halmashuri ya Wilaya ya Geita  ni kubwa na Halmashauri  inayo wajibu wa kupeleka kwa wananchi kwa kuwa bajeti hiyo imezingatia  kila kipaumbele katika utekelezaji.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Karia Rajab Magaro amelipongeza baraza hilo kwa namna ambavyo limeshirikiana na watumishi katika kufanya kazi na kupeleka makusanyo kutoka Bilioni 5 hadi kufika Bilioni 8 na kwenda kukusanya bilioni 11 kwa mwaka wa fedha 2025/26.

“Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anasisitiza tukusanye mapato ili Halmashauri ziweze kujitegemea hivyo niwaombe waheshimiwa madiwani  kuendelea kushirikiana  ili bajeti ziendelee kukua na kuwasaidia wananchi” Amesema Magaro.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Nag. Karia Magaro akizungumza katika mkutano maalum wa baraza la Madiwani wa kujadili mapendekezo ya mpango na bajeti kwa mwaka 2025/2026

Naye Katibu Tawala Wilaya ya Geita Bi Lucy Beda katika Baraza hilo ameipongeza Halmashauri kwa kuweza kufika asilimia 58.3 ya makusanyo  katika bajeti kwa mwaka wa fedha 2024/25 na kutoa wito kwa madiwani  kuendelea kuisimamia Halmashauri ili malengo ya utekelezaji yaweze kufikiwa. “Naamini bajeti hii iliyowekwa itakwenda kuwafikia wananchi” Amesema Bi Lucy Beda.

Aidha Katibu Tawala amemtaka Mkurugenzi Mtendaji na Watumishi wa Halmashauri kuendela kuibua vyanzo vingine vya mapato ili kuendelea kuwa na mapato makubwa. “Tunavyo vyanzo mbalimbali vya mapato tukavisimamie na kuibua vyanzo vingine ili kuendelea kuwa na mapato makubwa zaidi na kusimamia tulivyo navyo vema.” Ameongeza Bi Lucy Beda.

Pamoja na hayo Katibu Tawala ametoa wito kwa madiwani kuipa kipaumbele Kata ya Izumacheli iliyo kisiwani kufuatia kuwa na miundombinu duni ya barabara na kuielekeza  taasisi ya wakala wa barabara vijijini na mijini (TARURA) kuipa kipaumbele kata hiyo katika kuimarisha miundombinu ya barabara.


Waheshimiwa madiwani wakipitia rasimu ya bajeti katika mkutano maalum wa baraza la Madiwani wa kujadili mapendekezo ya mpango na bajeti kwa mwaka 2025/2026


Baraza hilo limeidhinisha jumla ya kiasi cha Tsh Bilionin 110.4 ambapo bajeti ya Halmashauri ni Bilioni 93.5, TARURA Bilioni 5.1 na RUWASA ni Bilioni 11.7 ambazo zitatumika katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa