• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAPITISHA BAJETI YA BILIONI 87.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

Posted on: January 24th, 2023

Na Michael Kashinde

Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Geita likiwa katika mkutano maalumu wa kujadili mpango na bajeti Januari 24, 2023 limejadili na  kupitisha bajeti ya kiasi cha shilingi bilioni 87.2 ikiwa ni makusanyo na matumizi kwa mwaka wa fedha 2023/2024.

Akiwasilisha mapendekezo ya mpango na bajeti katika mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Nzera Afisa Mipango Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bw. Walter Anthony amefafanua kuwa kiasi cha shilingi bilioni 15.08 ni fedha za ruzuku zitakazotumika kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo.

Bw. Walter ameeleza kuwa kiasi cha shilingi bilioni 2.5 ni ruzuku zitakazotumika kwa matumizi ya kawaida  (OC), shilingi bilioni 62.5 zitatumika kulipa mishahara ya watumishi, shilingi bilioni 6.3 ni makusanyo ya ndani ukiondoa mapato fungwa, na kiasi cha shilingi milioni 669.9 ni mapato mengine kama CHF, NHIF, na tozo za minara shuleni.

Miongoni mwa vipaumbele vilivyozingatiwa katika mpango na bajeti hiyo ni pamoja na kusimamia na kudhibiti ukusanyaji wa mapato kwa kununua POS mpya 40 na gari kwa ajili ya usimamizi na ufuatiliaji, sambamba na kuongeza miundo mbinu katika Sekta ya Elimu ambapo Halmashauri inatarajia kujenga shule tatu mpya na kukamilisha vyumba vya madarasa 70 kwa shule za msingi.

Aidha vipaumbele vingine ni pamoja na kuboresha minada ya Katoro, Bugalama, Kamena na Kakubilo pamoja na stendi za mabasi Rwamgasa, Nkome, Katoro na Nyarugusu ili kuongeza vyanzo vya mapato, sambamba na mapambano dhidi ya UKIMWI, Rushwa, uharibifu wa mazingira na unyanyasaji wa kijinsia (MTAKUWA).

Akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Geita Bw. Fredy Mhagama amewataka Waheshimiwa Madiwani ambao ni Wenyeviti wa Kamati za maendeleo za Kata kuendelea kuhamasisha ulinzi shirikishi katika maeneo yao ili kudhibiti vitendo vya wizi wa mifugo ambavyo vinafanyika katika baadhi ya maeneo.

Aidha Bw. Mhagama ametumia nafasi hiyo pia kuwataka viongozi kuanzia ngazi za vijiji kujenga utaratibu wa kuwasomea wananchi taarifa za mapato na matumizi katika maeneo yao ili kuepuka kuichonganisha Serikali na Wananchi huku akiwakumbusha Watendaji wa Kata kuacha kukaa na fedha za Serikali badala yake waziwasilishe Benki kama miongozo inavyowataka.

Akihtimisha kikao hicho cha siku moja Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe. Charles Kazungu ametoa wito kwa waheshimiwa madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita kuhakikisha wanahamasisha jamii katika maeneo yao kuwapeleka wanafunzi mashuleni ili kufikia jumatatu ya Januari 30, 2023 watoto wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza wawe wameripoti kwenye shule walizopangiwa kuendelea na masomo.

Halmashauri ya Wilaya ya Geita inatarajia kushirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo GGML, BUCKREEF, NELICO, PLAN INTERNATINAL, MDH, KIVULINI, SONGAMBELE, ICAP, CODERT,na SEDIT katika kuandaa na kutekeleza mpango na bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 uliopitishwa na baraza la madiwani wenye jumla ya kiasi cha shilingi 87,224,875,671.00

 PICHA ZAIDI


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa