• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMSHUKURU RAIS SAMIA SULUHU HASSAN KWA VYUMBA 267 VYA MADARASA YA SEKONDARI

Posted on: October 7th, 2022

Na. Michael Kashinde

Baraza la madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Geita Oktoba 7, 2022 limemshukuru Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia Halmashauri ya Wilaya Geita kiasi cha Tsh. 5,340,000,000 (Bilioni 5 na Milioni 340) kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 267 vya madarasa katika shule za Sekondari 39 kwa ajili ya kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka 2023.

Akitoa neno la shukrani katika mkutano maalumu wa baraza la Madiwani kwa niaba ya wajumbe wa baraza hilo, uongozi wa Chama Cha Mapinduzi na Serikali Wilaya ya Geita Mhe. Elisha Lupuga mwenyekiti wa kamati ya fedha, uchumi na mipango na diwani wa kata ya Bugulula, amesema kuwa viongozi, watumishi, na wananchi wa Halmashauri ya Wilaya Geita wanamshukuru sana Mhe. Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa nia yake njema ya kuwasaidia wanafunzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

“Mhe.Mwenyekiti tunaomba tuungane kwa pamoja wajumbe wote wa baraza hili ukiwemo Mhe. Mkuu wa Wilaya na viongozi wote wa Chama kuendelea kumshukuru Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa awamu ya Sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutupatia kiasi cha Tsh. 5,340,000,000."

Ameendelea kusema kuwa "hakika watumishi, viongozi na wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita wanamshukuru sana kutokana na nia yake njema kwa watoto wa Halmashauri yetu kwa kuwapatia vyumba 267 vya madarasa na ni matumaini yetu kuwa watoto wote watakaochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2023 watapata vyumba vya madarasa vyenye ubora na mandhari nzuri kwa niaba ya Halmashauri tunamshukuru sana Mhe. Rais.” amesema Mhe. Lupuga.

Kwa upande wake Mwl. Hossana Mussa Nshullo Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari Halmashauri ya Wilaya ya Geita akieleza mikakati ya utekelezaji wa ujenzi wa madarasa hayo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji, amesema kuwa timu ya Menejimenti imeazimia kutekeleza miradi hiyo kupitia Force Account ambapo pia zitaundwa kamati tano kwa ajili ya ufuatiliaji wa karibu wa miradi hiyo.

Mwl. Nshullo amebainisha kamati hizo kuwa ni pamoja na kamati ya usimamizi na ufuatiliaji ngazi ya Wilaya na Halmashauri, kamati ya usimamizi na ufuatiliaji ngazi ya Kata, kamati ya ujenzi ngazi ya shule, kamati ya manunuzi ngazi ya shule na Halmashauri na kamati ya Mapokezi ngazi ya shule na Halmashauri.

Halmashauri ya Wilaya ya Geita imeendelea kuchukua hatua mbalimbali kuelekea miradi hiyo ikiwa ni pamoja na maandalizi ya manunuzi ya vifaa vya viwandani ambayo yanaendelea kupitia kitengo cha manunuzi cha Halmashauri.

Aidha Halmashauri  inafanya tathmini ya maboma yote yaliyopo kwenye maeneo ya shule Mama na shule mpya zinazopendekezwa ili kujua thamani ya fedha iliyotumika huku mawasiliano na watendaji wa Kata yakiendelea ili kuwaagiza kuwasilisha Mihtasari ya mapendekezo ya maeneo ya kujenga shule mpya za Sekondari.

Miongoni mwa mapendekezo yaliyotolewa na timu ya menejimenti ni pamoja na kuwahamasisha wananchi walio kwenye maeneo ambayo shule mpya zitajengwa, kujitolea kujenga miundombinu mingine kama vile vyoo na huduma zingine zinazohitajika katika mazingira ya shule, kwa kuwa fedha zilizotolewa zimeelekezwa kujenga madarasa na samani peke yake.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Wilson Shimo akizungumza katika mkutano huo, amewataka wajumbe kuhakikisha wanaisaidia jamii hasa watoto kupata lishe bora ambayo ina mchango katika maendeleo ya wanafunzi kitaaluma huku akilitaja suala la lishe duni kuwa kikwazo kikubwa cha matokeo  mazuri kwa wanafunzi hasa wanapokaa muda mwingi bila kupata chakula wakiwa shuleni.

Aidha amewataka viongozi hao kuhakikisha wanatenga bajeti za chakula mashuleni huku akitoa wito  kwa viongozi hao na walimu kwa ujumla kuongeza bidii ili kuwasaidia wanafunzi hao kufaulu vizuri huku akikemea tabia za baadhi ya wazazi wanaowalaghai watoto wao hasa wa kike wafanye vibaya katika mitihani ili wasiendelee na shule ambapo wakati mwingine huwaozesha.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Geita Ndg. Barnabas Mapande ametumia nafasi hiyo kumpongeza Mkurugenzi Mtendaji Adv. John Wanga na timu ya menejiment Halmashauri ya Wilaya Geita kwa kazi nzuri wanazozifanya huku akitoa wito wa kusimamia vizuri ujenzi wa miradi hiyo ya madarasa ili thamani na ubora wake uonekane kama ilivyo dhamira ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan.

Mapande ametumia nafasi hiyo kutoa wito kwa wajumbe hao wanapozungumza na wananchi kuyasema wazi maendeleo yanayofanywa na Serikali kwa wananchi wake ili wananchi wajue, huku akishukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Geita.

Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita unaamini kuwa watoto wote watakaochaguliwa kujiunga na Kidato cha kwanza mwaka 2023 watapata vyumba vya madarasa vyenye ubora na mandhari nzuri, huku ukimuahidi Mhe. Rais pamoja na Serikali ya Mkoa na Wilaya kuwa, kazi hiyo ya ujenzi wa madarasa itafanyika kwa weledi, uadilifu na uwajibikaji wa hali ya juu.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa