• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

Posted on: April 30th, 2025

Nzera-Geita

Mkutano wa Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Geita umeendelea Aprili 30,2025 katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri Nzera baada ya tarehe 29,2025 kuwasilisha taarifa za utekelezaji wa shughuli za maendeleo ngazi ya kata. 

Akizungumza katika Baraza Hilo Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Karia Rajab Magaro ametoa pongezi kwa Waheshimiwa Madiwani kwa kusimamia jukumu la ukusanyaji wa mapato. 

"Waheshimiwa Madiwani mmekuwa bega kwa bega na Menejimenti katika kushauri na kusisitiza ukusanyaji  wa mapato ambapo hadi Machi  2025 Halmashauri imekusanya jumla ya Shilingi Bilioni 7.3 sawa na asilimia 88.26 ya mapato yanayotarajiwa kukusanywa kwa mwaka." Amesema Ndg. Magaro.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji amesema Halmashauri imepanga kusimamia na kutekeleza miradi yenye thamani ya shilingi  Bilioni 17.2 kutokana na mapato ya ndani , wahisani na Serikali kuu.

"Jumla ya Shilingi Bilioni 14.8 zimepokelewa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo kutoka Serikali kuu na wadau na Bilioni 3.1 kutoka mapato ya ndani."

Pamoja na hayo, Mkurugenzi Mtendaji ametoa rai kwa Waheshimiwa Madiwani kuendelea kusimamia utekelezaji wa miradi ili kupata thamani ya fedha.

"Niendelee kuomba Ushirikiano kwa Madiwani kujitoa ili kukamilisha na kuvuka  malengo kwa mpango wa 2024/2025." Amesema Ndg. Magari.

Aidha Ndg Magaro katika Mkutano huo wa Baraza la Madiwani Robo ya tatu, ameishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayo ongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kutoa fedha nyingi za miradi ya Maendeleo hali iliyopelekea kupunguza adha kwa wananchi.

Vilevile Ndg Magaro amewashukuru Waheshimiwa Wabunge, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa,  Mkuu wa Wilaya kwa Ushirikiano mzuri ambao wamekuwa wakiutoa ili Halmashauri iendelee kufanya vizuri katika nyanja zote.

Katika Baraza hilo Waheshimiwa Madiwani wameipongeza ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kwa kupata  Hati safi kutoka kwa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)

"Tuipongeze ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kwa kuipa Halmashauri Hati safi ya Hoja za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) amesema Mhe Hadija Said Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri.

Akihitimisha Kikao hicho cha Baraza Makamu Mwenyekiti Mhe Hadija Said amewashukuru Waheshimiwa Madiwani na Wataalam kwa namna walivyoshiriki Mkutano huo wa Baraza na kuwataka kuendelea kusimamia shughuli za maendeleo ikiwa ni pamoja na kufanya mikutano na wananchi katika maeneo yao.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa