• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

ASANTE SIKU YA MTOTO WA AFRIKA KWA KUJA NA HOSPITALI HALMASHAURI YA WILAYA GEITA

Posted on: June 16th, 2019

Wahenga walinena mtoto ni Baraka, kauli hiyo imejidhihilisha tarehe 16 june 2019 kwenye maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika ambapo Serikali inatarajia kuanza ujenzi wa hospitali nyingine ya Wilaya katika mji mdogo wa Katoro uliopo Halmashauri ya wilaya ya Geita.

Hayo yameelezwa na Mgeni rasmi kwenye siku hiyo ambaye ni Waziri wa Afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Ummy Mwalimu alipokuwa anajibu risala za viongozi mbalimbali akiwemo mkuu wa Mkoa Geita Mhandisi Robert Gabriel, amesema Kutokana na idadi kubwa ya watu, hospitali pekee iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Nzera haitokidhi hitaji.

Waziri Ummy amesema kuwa Serikali kupitia Wizara yake itatoa shilingi milioni 500 ili hospitali ianze kujengwa kwa haraka lakini pia amempongeza Mkuu wa mkoa wa Geita kwa kuahidi kutoa shilingi milioni 200 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo.

Kutokana na kanda ya ziwa kuwa na idadi ya watu takribani milioni 13.4 Waziri amesema haiwezi kuwa na hospitali 1 ya kanda (Bugando), hivyo Serikali imeamua kujenga hospitali nyingine ya rufaa ya kanda mkoani Geita ili kupunguza haja ya wagonjwa kwenda Bugando.

Amesema Serikali inampango wa kuifanya hospitali hiyo itakayojengwa Geita kuwa ndio kituo cha utalii wa matibabu katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania pia italenga kuwavutia Nchi za jirani kama Congo, Rwanda na Burundi kuja kupata matibabu hospitalini hapo.

Hata hivyo Katika kuhakikisha watoto wanalindwa na kupata haki zao za msingi amesema kuwa Serikali imechukua hatua mbalimbali kukabiliana na changamoto zinazowakabili watoto Nchini, pamoja na kuridhia mikataba ya kimataifa na kanda kuhusu haki na ustawi wa watoto,Serikali imeandaa mipango na mikakati mabalimbali inayolenga kuwalinda na kuwaendeleza watoto katika Nyanja zote.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa Geita Mhandisi Robert Gabriel amesisitiza kila mzazi kuhakikisha mtoto anapata mahitaji muhimu kama Elimu na afya bora pamoja na kulindwa, pia kuachana na dhana ya kusema mtoto wa kiume ni bora zaidi ya wakike kwani nyakati hizi viongozi mbalimbali Duniani ni wanawake na wanafanya vizuri.

Aidha mkuu wa mkoa alimuahidi mgeni rasmi kuwa mwisho wa mwaka huu anatarajia kukabidhi zahanati 100 zinazojengwa katika kila kijiji ambazo kwa sasa ujenzi wa maboma umefikia takribani asilimia 96.

Ujumbe wa maadhimisho ya siku ya motto wa Afrika kwa mwaka 2019, ‘Mtoto ni Msingi wa Taifa Endelevu, Tumtunze, Tumlinde, na kumuendeleza’, ambapo waziri Ummy alizindua kampeni ya kimataifa ya usawa kwa motto wa kike(Girls Get Equal) iliyoandaliwa na shirika la Plan International.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa